Maswali Mengine Yanayoulizwa Mimba

Je uaviaji mimba ni mbinu ya kuzuia uja uzito?

Mbinu za uaviaji mimba hazistahili kuchanganyishwa na mbinu za kuzuia mimba (mbinu za kupanga uzazi, ikijumuishwa na upangaji uzazi wa dharura). Mbinu za kupanga uzazi hufanya kazi kwa kuzuia kuachiliwa kwa ovari (kuachiliwa kwa yai) au kwa kuzuia yai na mbegu za kiume kukutana. Mbinu za kupanga uzazi, ikijumuisha upangaji uzazi wa dharura, haziwezi kutumika kutamatisha au kuhitilafiana na mimba iliyotungwa. Unaweza kutembelea www.findmymethod.org ili kujifunza mengi kuhusu mbinu za kupanga uzazi.

Kuna tofauti gani kati ya tembe ya kuavya mimba na tembe ya asubuhi – baadaye (upangaji uzazi wa dharura)?

Tembe za upangaji uzazi wa dharura (ECPs) ni salama na njia faafu za kuzuia mimba baada ya kujamiiana bila kinga. Hufanya kazi kwa kuzuia kuachiliwa kwa ovari (kuachiliwa kwa yai) au kwa kuzuia yai na mbegu za kiume kukutana. ECPs haziwezi kutamatisha ama kuhitilafiana na mimba iliyotungwa. ECPs ni tofauti na taratibu za kiafya zilizowekwa (ambazo hujumuisha mifepristone na misoprostol). Matibabu haya yana manufaa ya pekee kwa afya ya uzazi wa wanawake kote duniani.

Je matibabu ya uaviaji mimba ni sawa na tembe za kuavya mimba. Je matibabu ya uaviaji mimba ni sawa na uaviaji mimba kwa upasuaji?

Kuna njia mbili zitumikazo sana katika mbinu za uaviaji mimba
1) Matibabu ya uaviaji mimba: matibabu ya kuavya mimba hutumia madawa ya kibaolojia ili kutamatisha uja uzito. Wakati mwingine dhana “ uaviaji mimba pasi upasuaji” au uaviaji mimba kwa tembe” pia huwa zinatumika.
2) Uaviaji mimba kwa upasuaji: Katika taratibu za uaviaji mimba kwa upasuaji, mtaalamu aliyehitimu atamwaga uja uzito kutoka kwa tumbo la uzazi kupitia mlango wa uzazi ili kutamatisha uja uzito. Taratibu hizi hujumuisha ufyonzaji ombwe usiootomatiki (MVA) na upanuzi na uondoaji (D&E).

Je uaviaji mimba ni mbinu ya kuzuia uja uzito?

Mbinu za uaviaji mimba hazistahili kuchanganyishwa na mbinu za kuzuia mimba (mbinu za kupanga uzazi, ikijumuishwa na upangaji uzazi wa dharura). Mbinu za kupanga uzazi hufanya kazi kwa kuzuia kuachiliwa kwa ovari (kuachiliwa kwa yai) au kwa kuzuia yai na mbegu za kiume kukutana. Mbinu za kupanga uzazi, ikijumuisha upangaji uzazi wa dharura, haziwezi kutumika kutamatisha au kuhitilafiana na mimba iliyotungwa. Unaweza kutembelea www.findmymethod.org ili kujifunza mengi kuhusu mbinu za kupanga uzazi.

Kuna tofauti gani kati ya tembe ya kuavya mimba na tembe ya asubuhi – baadaye (upangaji uzazi wa dharura)?

Tembe za upangaji uzazi wa dharura (ECPs) ni salama na njia faafu za kuzuia mimba baada ya kujamiiana bila kinga. Hufanya kazi kwa kuzuia kuachiliwa kwa ovari (kuachiliwa kwa yai) au kwa kuzuia yai na mbegu za kiume kukutana. ECPs haziwezi kutamatisha ama kuhitilafiana na mimba iliyotungwa. ECPs ni tofauti na taratibu za kiafya zilizowekwa (ambazo hujumuisha mifepristone na misoprostol). Matibabu haya yana manufaa ya pekee kwa afya ya uzazi wa wanawake kote duniani.

Je matibabu ya uaviaji mimba ni sawa na tembe za kuavya mimba. Je matibabu ya uaviaji mimba ni sawa na uaviaji mimba kwa upasuaji?

Kuna njia mbili zitumikazo sana katika mbinu za uaviaji mimba
1) Matibabu ya uaviaji mimba: matibabu ya kuavya mimba hutumia madawa ya kibaolojia ili kutamatisha uja uzito. Wakati mwingine dhana “ uaviaji mimba pasi upasuaji” au uaviaji mimba kwa tembe” pia huwa zinatumika.
2) Uaviaji mimba kwa upasuaji: Katika taratibu za uaviaji mimba kwa upasuaji, mtaalamu aliyehitimu atamwaga uja uzito kutoka kwa tumbo la uzazi kupitia mlango wa uzazi ili kutamatisha uja uzito. Taratibu hizi hujumuisha ufyonzaji ombwe usiootomatiki (MVA) na upanuzi na uondoaji (D&E).

Naweza kuwafikia vipi kwa habari zaidi?

Kwa habari za ziada, unaweza kuwasiliana na timu yetu kwa info@howtouseabortionpill.org.

Marejeo

Tovuti hii inaweza kuhitaji kuki zisizojulikana na huduma anuwai za mtu mwingine ili iweze kufanya kazi kunavyotakikana. Unaweza kusoma Sheria na Masharti yetu na Sera za Faragha . Ukitaka kuendelea kutumia tovuti hii, ni sharti utupe idhini ili uweze kufanya hivyo.